Psalms 122

Sifa Kwa Yerusalemu

(Wimbo Wa Kwenda Juu. Wa Daudi)


1 aNilishangilia pamoja na wale walioniambia,
“Twende nyumbani ya Bwana.”

2 Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama
malangoni mwako.


3 bYerusalemu imejengwa vyema kama mji
ambao umeshikamanishwa pamoja.

4 cHuko ndiko makabila hukwea,
makabila ya Bwana,
kulisifu jina la Bwana kulingana na maagizo
waliopewa Israeli.

5 Huko viti vya enzi vya hukumu hukaa,
viti vya enzi vya nyumba ya Daudi.


6 dOmba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu:
“Wote wakupendao na wawe salama.

7 eAmani na iwepo ndani ya kuta zako
na usalama ndani ya ngome zako.”

8 Kwa ajili ya ndugu zangu na marafiki,
nitasema, “Amani iwe ndani yako.”

9 fKwa ajili ya nyumba ya Bwana Mwenyezi Mungu wetu,
nitatafuta mafanikio yako.
Copyright information for SwhKC